Jumatano, 30 Oktoba 2019
UJUMBE MFUPI WA LEO Na, Mwl Massawe
Jumapili, 27 Oktoba 2019
MAJINA YA WANAFUNZI WOTE WALIOPATA MIKOPO (HESLB)
http://www.unistoretz.com/magazine/heslb-batch-2-the-list-of-loan-beneficiaries-in-2019-2020-majina-ya-waliopata-mikopo-batch-2/
Jumamosi, 26 Oktoba 2019
FAHAMU UWEZO WA NDEGE MPYA YA ATCL (Boeing 787 Dreemliner) KUTOKA NCHINI MAREKANI
Ijumaa, 18 Oktoba 2019
HESLB MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MIKOPO 2019/2020
HESLB yatangaza majina ya wanafunzi waliopata mkopo wa elimu ya juu 2019/2020,
Download PDF hapa,
http://www.unistoretz.com/magazine/heslb-the-list-of-loan-beneficiaries-in-2019-2020-majina-ya-waliopata-mikopo-batch-1/
Alhamisi, 17 Oktoba 2019
HOW TO SUCCEEDED IN LIFE (Quote)
MAMBO MATANO YANAYOWEZA KUFUPISHA MAISHA YAKO, (Kusababisha uishi umri mfupi)
Jumanne, 15 Oktoba 2019
MAJINA YA WANAFUNZI KUMI BORA WALIOFAULU MTIHANI WA DARASA LA SABA 2019
https://results.necta.go.tz/results/2019/psle/psle.htm
MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA 2019,
MATOKEO YOTE BONNYEZA HAPA
Akitangaza matokeo hayo leo Jumanne Oktoba 15, 2019 Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk Charles Msonde amesema kwa jumla yanaonyesha ufaulu umeongezeka kwa asililia 3.78 lakini ufaulu katika somo la Kiingereza bado ni mdogo likilinganishwa na masomo mengine.
"Ufaulu katika somo la Kiingereza unaendelea kuimarika mwaka hadi mwaka hivyo juhudi za makusudi zinahitajika kuendelea kufanyika ili kuinua kiwango cha ufaulu katika somo hili," amesema Dk Msonde.
Aidha katika matokeo hayo, Grace Imori Manga wa shule ya msingi Graiyaki ya mkoani Mara ametangazwa kuwa wa kwanza kitaifa akifuatiwa na Francis Gwani wa shule ya msingi Paradise ya mkoani Geita na namba tatu imeshikiliwa na Loi Kitundu wa Shule ya msingi Mbezi ya Dar es Salaam.
Wengine katika orodha ya 10 bora ni Victor Godfrey wa shule ya msingi Graiyaki, Azizi Yassin wa Graiyaki goldie Hhayuma wa Graiyaki, Daniel Daniel wa shule ya msingi Little Mkoani Shinyanga, Hilary Nassor wa Peaceland ya Mwanza, Mbelele Mbelele wa Kwema Modern ya Shinyanga na Nyanswi Richard wa Graiyaki ya Mara.
Shule 10 bora kitaifa ni Graiyaki ya Mara, Twibhoki ya Mara, Kemebos ya Kagera, Little Treasures ya Shinyanga, Musabe ya Mwanza, Tulele ya Mwanza, Kwema Morden ya Shinyanga, Peaceland ya Mwanza, Mugini ya Mwanza na Rocken Hill ya Shinyanga.
Kimkoa, Mkoa wa Dar es Salaam umeshika namba moja ukifuatiwa na Arusha, Iringa, Kagera, Katavi, Kilimanjaro, Mbeya, Simiyu, Njombe na Pwani.
Halmashauri 10 bora zimeongozwa na Arusha jiji, Ilemela, Kinondoni, Mwanza jiji, Ilala Manispaa, Moshi Manispaa, Bukoba Manispaa, Iringa Manispaa, Biharamulo na Arusha
https://results.necta.go.tz/results/2019/psle/psle.htm
KAULI TANO ZA KUKUONGOZA UNAPOKUA KAZINI
A,Kuna maisha baada ya kazi unayoifanya, heshimu kipato chako na usimdharau mtu kwa nafasi uliyonayo,
B,Fanya jambo kwa nafasi yako siyo kwa kuiga, angalia nafasi yako katika kusaidia na kufanya kitu Fulani,Kama mwenzako kafanya makubwa na huna uwezo was kufanya kama yeye usilazimishe,
C.Penda kazi yako angalia ulipotoka na usifuate makundi, kumbuka kazi uliomba mwenyewe na ukafika mwenyewe marafiki uliowakuta kazini wasibadili tabia yako na kukufanya upotee kwani mwisho wa Sik kila mmoja atarudi alipotoka,
D.Busara yako ikuongoze katika mambo yako kazini, kabla hujachangia chochote fikiria kwanza ubora na udhaifu was kile unachoenda kukiongea ndipo utoe hoja kukosoa au kuunga mkono,
E. Tii mamlaka iliyoko juu yako, tii viongozi wako na Fanya kazi pasipo kuangalia udhaifu wao kwani hata maandiko matakatifu yanasema tiini mamlaka iliyo kuu kwani mamlaka zote zimewekwa na Mungu,
Kwa elimu na mafunzo mbalimbali ya namna ya kufanikiwa tucheki SMS/WhatsApp no: 0710843184
Mwl Innocent Massawe Priscus
HISTORIA YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE (BABA WA TAIFA)
Alikuwa mojawapo kati watoto 26 wa Nyerere Burito, chifu wa kabila la Wazanaki. Alipokuwa mtoto Nyerere alichunga mifugo ya babake; katika umri wa miaka 12 aliingia shule akitembea kilomita 30 hadi Musoma. Baada ya kumaliza shule ya msingi aliendelea kusom
a shule ya wamisionari Wakatoliki huko Tabora. Katika umri wa miaka 20 alibatizwa akawa mkristo Mkatoliki hadi mwisho wa maisha yake.
(Mama Maria Nyerere, mke wa Hayati baba wa Taifa)
Mapadre wakaona akili yake wakamsaidia kusoma ualimu huko Makerere, Kampala, Uganda kuanzia 1943 - 1945. Makerere akaanzisha tawi la Umoja wa wanafunzi Watanganyika pia amejihusisha na tawi la Tanganyika African Association (TAA). Baada ya kumaliza masomo ya ualimu alirudi Tabora akifundisha shule ya St.Mary´s. Mwaka 1949 alipata skolashipu ya kwenda kusoma kwenye Chuo Kikuu cha Edinburgh huko Uskoti / Uingereza akasoma M.A. ya historia na uchumi(alikuwa mtanzania wa kwanza kusoma katika chuo kikuu cha Uingereza na mtanzania wa pili kupata shahada ya elimu ya juu nje ya Tanzania).
Aliporejea Tanganyika kutoka masomoni, Nyerere alifundisha Historia, Kingereza na Kiswahili katika shule ya St. Francis iliyo karibu na Dar es Salaam. Mwaka 1953 alichaguliwa kuwa raisi wa chama cha Tanganyika African Association (TAA), cham
a ambacho alikisaidia kukijenga alipokuwa mwanafunzi katika chuo kikuu cha Makerere. Mwaka 1954 alikibadilisha chama cha TAA kwenda katika chama cha Tanganyika African National Union (TANU) ambacho kilikuwa cha kisiasa zaidi kuliko TAA. Ndani ya mwaka mmoja chama cha TANU kilikuwa tayari chama cha siasa kinachoongoza Tanganyika.
Uwezo wa mwl. Nyerere uliwashitua uongozi wa kikoloni na kumlazimisha Nyerere kuchagua kati ya siasa na kazi ya ualimu. Nyerere alisikika akisema kuwa alikuwa mwalimu kwa kuchagua na mwanasiasa kwa bahati mbaya. Alijiuzuru ualimu na kuzunguka nchini Tanganyika kuzungumza na watu wa kawaida na machifu ili kuleta muungano katika mapigano ya uhuru. Pia alizungumza kwa niaba ya TANU katika Trusteeship council na Fourth committee ya Umoja wa Mataifa (UN) huko New York. Uwezo wake wa kimaongezi na kuunganisha watu ulimwezesha kufanikisha Tanganyika kupata uhuru bila umwagaji wa damu.
Ushirikiano mzuri aliouonyesha aliyekuwa gavana wa wakati huo bwana Richard Turnbull ulisaidia pia kuharakisha upatikanaji wa uhuru. Nyerere aliingia katika bunge la kikoloni mwaka 1958 na kuchaguliwa kuwa waziri mkuu mwaka 1960. Mwaka 1961 Tanganyika ilipata uhuru wake na tarehe 9/12/1961 Nyerere alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Tanganyika huru na mwaka mmoja baadae Nyerere alikuwa raisi wa kwanza wa jamhuri ya Tanganyika. Nyerere alikuwa kiungo muhimu katika katika muungano wa Tanganyika na Zanzibar kutengeneza Tanzania baada ya mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964 yaliyomtoa madarakani sultani wa Zanzibar Jamshid bin Abdullah.
Sifa zake
Bado anakumbukwa na watanzania hasa wa hali ya chini kutokana na sera zake za kujali utu na ubinadamu.Pia ataendelea kukumbukwa na waafrika kote barani hasa kwa mchango wake mkubwa wakati wa harakati za kupigania uhuru katika nchi mbali mbali barani Afrika.
Ni mmoja wa viongozi wachache wanaokumbukwa kwa kutojilimbikizia mali pamoja na kutawala kwa miaka zaidi ya 24.
Mwishoni mwa maisha yake Nyerere aliishi kama mkulima wa kawaida kijijini kwake Butiama. Alipatwa na kansa ya damu (leukemia) na kufariki Uingereza wakati wa kutibiwa katika mji wa London tarehe 14 Oktoba, 1999. Alizikwa mahali pa kuzaliwa kwake, kijiji cha Butiama.
(Kaburi la Baba wa Taifa)
Watanzania tumempoteza kiongozi mpiganaji na mwenye uchungu na nchi yake, aliepinga vita dhidi ya umasikini, ubaguzi na rushwa. Hamna kiongozi mwengine alieiga mfano wa Baba wa Taifa tumebakiwa na viongozi wenye uchu na madaraka kujirumbukizia mali wao na familia zako ni aibu sana kwa Taifa maana enzi za Mwalimu hapakukuwa na hali hii ya kiongozi kumiliki mali nyingi mfano mzuri alionesha yeye ambae hakuwa na uchu wa kujirumbikizia mali ingawa alikuwa na nafasi kubwa na inayomfanya aweze kufanya hivyo lakini alikuwa na uzalendo na nchi yake. Nchi sasa inapoteza dira hamna viongozi bora ila kuna bora viongozi aibu kwa Watanzania.
AINA ZA WATU NA TABIA ZAO KATIKA KIPATO NA MAFANIKIO
Leo nakuletea aina tatu za watu katika tofauti katika kipato pamoja na tabia zao,
,Katika maisha yetu ya kila Siku tuna aina tatu za watu kulingana na kipato chao ambao ni hawa wafuatao;
A,Watu wenye kipato cha juu,
B,Watu wenye kipato cha kati,
C,Watu wenye kipato cha chini,
Hayo ndiyo makundi makuu ya kipato katika Dunia hii ya Teknolojia, Kiufupi tutazame sifa/tabia za kila kundi,
A.WATU WENYE KIPATO CHA JUU;
za hawa hutumia kipato walichonacho kuzalisha kipato kingine, Mfano anamoliki Kampuni kubwa fedha anazozipata huzitumia kufungua kampuni nyingine ndogo.
Pia hawa huweka akiba na kwa kawaida huendelea kukua na kufanikiwa zaidi kutokana na kuwa na vyanzo vingi vya mapato,
Tabia nyingine huwa ni wavumilivu, wenye subira, wanajali na wapo makini katika kusimamia miradi yao vilevile wana uhusiano mzuri sana na jamii inayo wazunguka,
Tabia ya mwisho watu hawa hutumia muda wote 24 hrs kuzalisha na huwa na dharura nyingi wanapo alikwa katika sherehe au matamasha kutokana na huwa bize sana,
B.WATU WENYE KIPATO CHA KATI
Hawa tunao kwa wastani katika mazingira yetu na huwa wana tabia zinazo shabihiana na za wale wenye kipato cha juu na maranyingi huweza kufikia kipato cha juu kirahisi, Hawa hupenda kuzalisha Mali pia baadhi hupenda starehe za wastani na muda mwingi huutumia katika kuzalisha na starehe, ni rahisi sana hawa kutajirika pia ni rahisi kufilisika,
Katika hatua hii wengi huwekeza katika asset mbalimbali kama mashamba/viwanja nyumba/majengo n.k
C.WATU WENYE KIPATO CHA CHINI
Hawa ndio wenye kundi kubwa Duniani, watu hawa wana sifa nyingi zinazowafanya kuendelea kuwa maskini;
1.Wavivu kufanya kazi na hupenda kuajiriwa kuliko kujiajiri wenyewe hulala sana na hupenda starehe, hunununa mapambo mengi ya ndani na vikorokoro vingi vya nyumbani,pia hawana akiba na hufanya matumizi makubwa bila mipango, humiliki vitu vya anasa visivyozalisha kama nguo,n.k
2.Kwakawaida watu hawa hawatumii kipato chao kuzalisha kipato kingine hivyo hubaki katika umasikini wao daima,
MWISHO; Kila mtu alizaliwa maskini lakini siyo kila MTU atakufa maskini, hii ni kutokana na mfumo wa maisha yako, Badili mtazamo wako sasa na Ishi kitaalamu ukiiona kesho iliyo bora kuliko Leo,
Kwa msaada wa kijasiriamali wasiliana nasi
0710843184/0753352264
Mwl wako INNOCENT M PRISCUS
Jumapili, 13 Oktoba 2019
SIKU TATU ZAONGEZWA KATIKA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA
WAZIRI wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo ameongeza siku tatu kwa wananchi kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24 Mwaka huu.
Jafo awachongea Ma-RC kwa Rais
Stars kamili yawasili Kigali
MCT yaboresha tuzo uandishi wa habari
Mvua zasababisha madhara makubwa HABARI KUBWA Akizungumza kabla ya kujiandikisha Kijijini kwake Kimani,Kisarawe mkoani Pwani leo, Waziri Jafo alisema kuongezwa kwa siku tatu hizo kumetokana na sababu mbalimbali ambazo kimsingi zimesababisha wananchi kuikosa fursa hiyo.
Alisema kimsingi siku za uandikishaji huo zilizoongezwa kutoka leo hadi Oktoba 17, kumesabishwa na tatizo la mvua zinazoendelea kunyesha katika mikoa mbalimbali na hivyo kuleta shida kwa wananchi wengi kujiandikisha.
Aliitaja sababu nyingine kuwa ni pamoja na uwepo wa zoezi la wananchi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, hali iliyoleta dhana kwa baadhi ya wananchi kuwa kitambulisho cha mpiga kura kitawawezesha kupiga kura katika uchaguzi huo wa Serikali za mitaa.
"Kutokana na sababu hizo na kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa za Mwaka 2019 na matangazo ya Serikali Na 371,372,373 na 374 ya Mwaka 2019 Waziri mwenye dhamana na Serikali za mitaa ana mamlaka ya kutoa miongozo mbalimbali kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa" alisema Jafo
Alisema kutokana na kanuni hizo na changamoto zilizojitokeza Wizara yake imeona vyema kuongeza siku hizo tatu ili kuwapa nafasi wananchi kujiandikisha na hivyo kutumia fursa yao ya kikatiba kuwachagua viongozi wanaowataka.
Aidha alisema tangu kuanza kwa Oktoba 8 hadi Octoba 12 Mwaka huu wananchi zaidi ya Milioni 11 walikuwa tayari wamejiandikisha nchi nzima kushiriki uchaguzi huo huku akilitaja zoezi hilo kuwa lenye mafanikio makubwa ikilinganishwa na kipindi kingine chote.
Alisema kufuatia mabadiliko, ratiba ya uandikishaji wa orodha ya wapiga kura na matukio yanayohusu uandikishanji yatakuwa na mabadiliko fulani fulani ikiwemo kubandikwa kwa orodha ya wapiga kura litakalofanyika kuanzia Oktoba 18, utoaji wa pingamizi kuhusu uandikishaji wapiga kura litakalofanyika Oktoba 14 hadi 24.Mabadiliko mengine ni pamoja na uamuzi kuhusu pingamizi litalofanyika kuanzia Oktoba 24 hadi 25,marekebisho ya orodha ya wapiga kura kuanziaa Oktoba 25 hadi 25 pamoja na ukataji wa rufaa dhidi ya uamuzi wa pingamizi utakaofanyika Oktoba 24 hadi 26 sambamba na ukataji wa rufaa utakaofanyika Oktoba 24 hadi 29 Mwaka huu.
Aidha alisema matukio mengine yote zikiwemo kampeni za wagombea zitaendelea kubaki kama kawaida huku akiwataka wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili kuwa na sifa ya kupiga kura katika uchaguzi huo. 13 OCT 2019
NAMNA YA KUMFURAHISHA MPENZI WAKO
TENDO la ndoa (kwa wanandoa) si tu linatumika kuboresha uhusiano kati ya mume na mke bali pia ni dawa inayoweza kuutibu mwili, akili na hisia. Hata hivyo, lazima liwe ni tendo lililokamilika, kwa maana lazima mwanaume na mwanamke wote walifurahie na kuridhika.
Tendo hili lisipofanyika kwa ukamilifu wake, hubadilika na kuwa kero kubwa na janga kwa wanandoa. Kama ambavyo nimekuwa nikieleza mara kwa mara, sidhani kama yupo mtu ambaye hataki kumfurahisha mwenzi wake wawapo faragha.
Tatizo ni kwamba wengi hawana maarifa ya nini cha kufanya awapo faragha na mwenzi wake, na matokeo yake wamekuwa wakijiendea wanavyoweza, kama kutembea kwenye giza totoro usiku wa manane.
Hakuna mahali ambapo unaweza kufundishwa namna ya kumfurahisha mumeo au mkeo, angalau kidogo wazee wetu enzi zao walikuwa wanapelekwa jandoni na unyagoni, siku hizi unakuja kujifunzia ndani ya ndoa, yaani kama ni mechi ya mpira wa miguu basi unajifunzia kutuliza mpira na kupiga danadana uwanjani wakati wa mechi ambayo ni lazima ushinde.
M f a n o mwepesi ambao huwa napenda kuutumia ni kwamba kila mtu anaweza kuwa anatamani kupiga gitaa na kuzalisha muziki mzuri, lakini hebu jiulize, kama hujawahi kujifunza kupiga gitaa na ukaelewa, ukipewa gitaa sasa hivi unaweza kupiga na kutoa muziki mzuri? Jibu ni HAPANA.
Mapenzi ni sanaa, lazima ukubali kujifunza na kuyatafuta maarifa mahali popote yalipo ili uwe bora, huyo uliyenaye unaweza kuwa unafanya kila kitu kwa ajili yake, unajitahidi kumuonyesha upendo wa hali ya juu lakini kama hujui nini cha kufanya muwapo faragha ili afurahi, ni sawa na kazi bure. Ni kwa msingi huo ndiyo maana nikaamua tujadiliane mada hii kama inavyojieleza hapo juu.
MAANDALIZI YA KIHISIA
Jambo la kwanza ambalo unatakiwa kulifahamu, ni kwamba ili mume au mke afurahie tendo muwapo faragha, lazima awe ametulia kihisia. Haiwezekani mmetoka kukwazana kuhusu jambo fulani, hamjapata suluhu na kila mmoja ana hasira halafu ndiyo mnaingia uwanjani, hamuwezi kufurahia tendo kwa mtindo huo na hii inawahusu wote.
Maandalizi mazuri ya tendo yanaanzia katika maelewano, mpokee vizuri kwa maneno yaliyojaa bashasha, kwa sauti ya upole, mbembeleze, mpetipeti na msifie! Ukiikamilisha kwa ukamilifu hatua hii ya kwanza na ya muhimu, basi utakuwa tayari umeshamuingiza kwenye safari ya kuelekea kufurahia tendo.
Mnapokuwa eneo la tukio, hutakiwi kuwa na papara! Lazima kwanza na wewe akili yako uitulize na badala ya kukimbilia kuingia mchezoni na kuanza kupiga mbizi kama mtu anayejifunza kuogelea, unatakiwa kwanza kutumia muda wa kutosha kupasha misuli moto.
Muda unaoshauriwa kitaalamu, ni angalau dakika thelathini
ndani ya muda huu mfanyie yale mambo yatakayoamsha hisia zake za ndani, viungo vya mwili wako kama mikono, vidole, mdomo, masikio vinaweza kuzalisha hisia nzuri sana kama utakuwa unajua nini unatakiwa kufanya kwa wakati gani.
Narudia tena, epuka kuwa na papara za kukimbilia uwanjani, maandalizi ni muhimu sana kwani yatamuandaa mwenzi wako kimwili na kihisia. Ukiwa na uhakika kwamba maandalizi yamefanyika kwa ukamilifu, sasa unaruhusiwa kuendelea na hatua kubwa na ya muhimu inayofuatia.
Katika hatua hii ambayo kimsingi ndiyo inayowaunganisha, pia unatakiwa kuwa na uelewa juu ya nini cha kufanya na kwa mtindo gani, siyo unaingia kwa papara kama unakimbizwa, hapana. Hapa pia unatakiwa kujifunza zaidi ili kuhakikisha unaibuka mshindi kwa kumfikisha mwenzi wako kwenye kilele cha safari yake ya huba.
Jumapili, 1 Septemba 2019
KAMA UNATAKA KUWA MASIKINI FANYA HAYA
Ndugu kama unataka kubaki katika umasikini wako Fanya haya yafuatayo;-
1.Usiamke mapema.
2. Usipange matumizi ya Pesa zako.
3. Usiweke akiba mpaka utakapo-kuwa tajiri.
4. Chagua kazi. Mimi nimesoma siwezi kufanya hii kazi.
5. Usifikirie kuanzisha biashara mpaka malaika akishuka kutoka mbinguni na kukukabidhi mtaji.
6. Endelea kuilahumu serikali na wazazi ambao hawakukupa Elimu.
7. Tumia Pesa nyingi kuliko kipato chako.
8. Hakikisha unaenda na fashion. Kila toleo jipya la nguo, viatu, simu lazima na wewe ununue.
9. Wanunulie watoto wako chochote watakacho kuomba.
10. Endelea kutumia muda mwingi zaidi kwenye social networks. Kama Whatsapp, Facebook na Instagram,
N:B Ukitaka kuondokana na Umasikini nenda kinyume na hayo yote
"AHSANTE"
Ijumaa, 23 Agosti 2019
TABIA ZA KUKWEPA ILI UFANIKIWE KIJASIRIAMALI NA KIMAISHA
Usikae bila shughuli yeyote
Epuka uvivu, Buni Kitu kitakachokupa fedha yaani shughuli ambayo ita kukeep busy, kwa kiwango kidogo
Usidharau ulivyo navyo
Haijalishi ni kidogo kiasi gani focus katika maono chanya kipende,kiheshimu, ongeza ubunifu na ukikuze,
Acha visingizio
Mafanikio ya mtu humtegemea yeye kwa 90%, Mafanikio yako yapo ndani yako, Usimlaumu au kumsingizia mtu.
Usiahidi uongo na usidhulumu MTU
Ukitoa ahadi hakikisha unatekeleza na pia tenda haki, hapa tunazungumzia "Mahusiano" Jenga mahusiano mazuri na jamii inayokuzunguka kwani jamii yako ndiyo maendeleo yako
Usiwe tegemezi wa mawazo
Usiishi kwa mazoea,kufuata mkumbo au kufuata wanachotaka wengine, "Fanya unacho amini kuwa ni sawa"
Usikate tamaa
Unapokutana na magumu pambana nayo, unapo anguka simama, unapokosea jifunze, songa mbele na kamwe usiwe na woga,
Nikutakie utekelezaji mwema,
Mwl Massawe,
Ijumaa, 9 Agosti 2019
KABLA HUJARIPOTI CHUO SOMA HII
Mkumbushe ndugu au rafiki yako kuwa maisha ya CHUO ni sawa na BONGO MOVIE watu wengi huigiza. Hata yule wa MBEYA vijijin atasema kwao MWANZA....
1. Mwambie anaenda kusomea taaluma sio kazi. Anaweza kusoma uhasibu akawa dobi...Anaweza somea Ualimu akawa mhudumu wa Bar au boda boda
2. Mwambie Kufaulu Taaluma sio Kufaulu maisha.wapo watu wenye elimu kumzid yeye ila hawana ajira. Hata wenye ajira bado maisha magumu
3. Mwambie Kupata alama nyingi sio kujua mambo mengi.... Wapo walio kuwa wanashika nafas za kwanza darasan ila leo Wanazidiwa uchumi na wenzao walio onekana hawana akili
4. Mwambie akifika chuo atakutana na watu wa mikoa tofauti na hata majiji. Ila akumbuke anatokea kijijini au wilaya iliyo duni, tena kule ndanindani... Hivyo asijikweze ili aonekane
5. Mwambie Marafiki wa chuo hubadilika kila baada ya semester. Kuendelea kung'ang'ania wale wa awali ataisoma namba....Akumbuke chuo ndiko mlokole hujifunza kwenda Club..kulewa na kuvaa nguo za ajabu
6. *Mwambie semester1 atakuwa na wapenzi wengi sana ila atumie kinga kwa gharama yoyote ile.* ..kama ni wakike akumbuke anasubiriwa na wale wa mwaka wa 2 na 3 ili asajiliwe ktk orodha ya Kontena jipya....
7. Mwambie makundi makundi chuoni humaliza hundi mfukoni... Atapata marafiki wapeta starehe. Pesa zake zitaisha
8. Mwambie Boom huwa linakuja ila Laki5 ya chuoni sio Laki5 ya nyumbani....hela ya chuoni huisha haraka na bila mpangilio hivyo awe makin ktk matumiz yake
9. Mwambie chuoni hakuna. NDOA ila kuna uzinzi.. Hivyo aachane kubeba majukum ya ndoa ikiwa kaenda kusoma. Mwambie kuishi kiunyumba na girl au boy kama wana ndoa sio ujanja ila ni ulimbuken na kesho ataumbuka
10. Mwambie awe na msimamo na asikurupuke kuanzisha mahusiano chuon ikiwa nyumban ana mtu anae mpenda kwa dhat.. Chuon kuna watu wapo kuharibu Malengo ya wengine awe makin
11. Mwambie wahadhiri (Lecturers) wa kitanzania wanatamaa ya ngono hivyo akiwa mvivu darasan bas atafeli na ili apewe Marks itabid awe tayar kumvulia chupi kila muhadhir ambao weng wao wagonjwa
12. Mwambie Chuoni kuna Makanisa na Misikiti. Wanafunzi ni zaidi ya 1000 lakini waumini ni wachache. Akumbuke kusali.
13. Mwambie kama ni wa kike kuwa aridhike na hali ya nyumban. Asifikirie kutafuta SPONSOR ili kupunguza ugum wa maisha .. Atajiingiza ktk matatizo makubwa
14. Mwambie kuwa asiwadharau watu alio soma nao nyuma kisa hawajapata nafas kufika chuo.. Siku akimaliza chuo wapo atao wakuta wana biashara kubwa hivyo kumpa kibarua
15. Mwambie Simu na nguo za gharama ni muhimu lakini sio lazima... Hivyo asipende tumia vibaya pesa ambayo anapewa kwa awamu mana siku atazikumbuka akimaliza masomo
16. Mwambie marafiki wanaokuwa naye kipindi hana hela asiwasahau... Awaepuke marafik wanafik wanao mfundisha kutafuta wanawake au wanaume
17. Mwambie chuoni ni sehemu ya kutengeneza Connection na watu muhimu...akae mbali na watu wasio msaada kwake
18. Mwambie chuoni kuna watumishi wanao jiendeleza..husoma huku wakiendelea kupokea mshahara wengi wao ni waume na wake za watu.. Hawa ndo wanao tumia pesa zao kulaghai mabint na vijana
19.Mwambie pia baada ya kumaliza chuo haina maana amefanikiwa maisha. Hapa ndipo msoto mpya unapoanzia... Anapo waona kaka na dada zake wamemaliza chuo ila wapo tu mtaan asifikir ni wazembe ila usawa na mfumo unabana
20. Mwambie Maisha ni mafupi sana Adumu kumcha Mungu na kufanya mambo mazurii, Lastly Asimdharau mtu yeyote.,....Akumbuke na azingatie kuwa kuna maisha baada ya chuo...
Asijisahau sana maana mtaani kugumu.. Mabinti wenye DEGREE wana amua kuolewa na vibabu nao vijana kutembea na wazee sababu ya kukosa ajira....
Atambua kuwa leo hii dreva boda boda au bajaji ana uhakika wa kuilisha familia yake kila siku kuliko muhitimu wa chuo kikuu. Hivyo asiwe na dharau kuwa hawez olewa na mtu mwenye elimu ya chini
Pia akumbuke sio kila dreva au konda hajasoma..watu wana vyeti vyao na ufaulu mzur
Kama haelewi basi tumuache
Tumsubiri akimaliza.
IKIKUFAA IFANYIE KAZI
MUNGU AWAONGOZE KATIKA NJIA ILYOSAHIHI NA AWAPE UJUZI UTAKAOWASAIDIA ATA KAMA WATAKOSA AJIRA.
Ameen..
#enterprenuership
#invest_on_time.
#invest_for_ur_future
TANZANIA INA FURSA GANI ZA BIASHARA?
Habari,
Leo nakuletea Fursa za Biashara ambazo Tunaishi Nazo Tanzania,na wengi tumekua hatuzitumii.
Zipo Fursa nyingi katika sekta mbalimbali kama; Kilimo,uchuuzi,usindikaji,kutengeneza bidhaa n.k
Leo nakupa kwa uchache Fursa za biashara ndogondogo Tanzania ambazo unaweza kuzitumia na ukabadili maisha yako.
1.Kutengeneza Mifumo inayotumia mtandao, (APPS) Mifumo hii inaweza kuwa mahususi kwa Huduma mbalimbali kama starehe/burudani,Biashara,Huduma za kijamii n.k
2.Ufugaji; hapa tunaangalia Ufugaji mdogo wa Mbuzi wa kisasa,kuku chotara,samaki,sungura,unenepeshaji ng'ombe n.k
3.Kilimo Biashara; Kilimo hiki kinategemea na hitaji la watu ila best ni "Mboga za Majani" hiki ni Kilimo ambacho soko lake ni kubwa Tanzania, pia unaweza kulima Papai,Tangawizi,Miche ya miti,n.k Kikubwa endana na uhitaji wa eneo ulilopo,
4.Usindikaji; Pia unaweza kusindika Asali,Viungo mbalimbali,Mafuta yatokanayo na matunda,n.k Chukua malighafi mtaani na uiongezee thamani kisha irudishe sokoni,
5.Huduma za usafiri; Katika kipengele hiki nitazungumzia juu ya kukodisha usafiri kama pikipiki au baiskeli kwa maeneo ya vijijini, na mijini, Kuwa wakala wa kampuni/mtu kutafuta wateja (Dalali) n.k
6.Huduma za Miamala ya simu; Hii ni Fursa Muhimu pia kuwa Wakala wa Tigo,Vodacom,Airtel n.k kuweka na kutoa fedha kusajili line na kutatua changamoto za mtandao,
7.Huduma ya kibanda umiza; Namaanisha kibanda cha kuonyeshea Movies,Mipira mbalimbali ya TPL,Afcon,EPL,UEFA n.k Pia katika kibanda hiki unaweza kuwa na Huduma za kucharge simu,kuuza vocha na kuuza vinywaji baridi
8.Huduma ya Genge; Genge pia huweza kubadili maisha yako tengeneza Genge uza mbogamboga kama, Dagaa, samaki,mchicha,ndizi,matunda mengne kama maembe,machungwa pia boresha uza mikate, n.k
9.Huduma ya Bites (mjini); Bites ni muhimu hasa maeneo ya stand za mabus unaweza tengeneza sehem ya kuuza vikorokoro mbalimbali vya kukaanga na uka make money, Hapa yaweza kuwa,Karanga,popcon,kuku,vusheti,crips,chips,n.k
10.Huduma ya maji,juice na urembo vituo vya mabus; Wapo wengi wanauza hivi vitu na ukitulia na kufanya Biashara vizuri hakika hutabeba lile boksi LA maji miaka miwili lazima uwe na mtaji
All the best
Kwa msaada Kibiashara nitafute hapa,
0710843184
Alhamisi, 8 Agosti 2019
FAIDA CHACHE ZA MWANAMKE MJAMZITO KUSHIRIKI TENDO LA NDOA
Kuna watu wamekua wakiuliza mara kwa mara kama inaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka umri gani wa mimba au ni sahihi kufanya tendo la ndoa kipindi cha ujauzito? maswali yalikua mengi sana hivyo leo nimeamua nijibu maswali hayo na makala hii.
Mwanamke akiwa na mimba anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa hata kama anatarajia kuzaa kesho yake, hakuna tatizo lolote linalomzuia kufanya hivyo, baadhi ya wanawake wamekua wazito sana kufanya hivyo kwa kua na sababu mbalimbali za kujitetea bila kujua kwamba wanazikosa faida hizi ambazo ni muhumu kiafya. Faida zenyewe ni kama zifuatazo;
Husaidia uchungu mzuri na kupona mapema;
Kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa huambatana na kubana kwa misuli ya nyonga hii husaidia kuweka imara misuli ya nyonga ambayo ni muhimu sana wakati wa kusukuma mtoto na baada ya kuzaa kwani misuli hii ikiwa legevu mwanamke huweza kushindwa kuzaa kwa njia ya kawaida na hata baada ya kuzaa huweza kushindwa kuzuia mkojo usitoke wenyewe au kuvuja damu kwa muda mrefu.
Hupunguza kwenda ovyo kukojoa au kujikojolea ;
Wakati wa ujauzito mtoto anapozidi kua mkubwa anazidi kukandamiza kibovu cha mkojo, hii humfanya mama aende chooni kukojoa mara kwa mara na wakati mwingine hata akipiga chafya au kukohoa basi mkojo unaweza kutoka wenyewe. tendo la ndoa huibana misuli ya nyonga na kuzuia hali hii.
Huzuia uwezekano wa kupata kifafa cha mimba; Tafiti zinaonyesha kwamba aina ya protini inayopatikana kwenye mbegu za mwanaume huongeza kinga ya mwili na kuzuia uwezekano wa kupata kifafa cha mimba ambacho kinaua wanawake wengi sana.
Hutibu tatizo la kufika kileleni kwa shida;
Kipindi cha ujauzito chuchu za mwanamke na kinembe chake huvimba na kuongezeka hisia mara dufu huku kiwango cha homoni za oestrogen kikiwa juu sana, hii humfanya kufika kileleni kirahisi sana kuliko mwanzoni.
Huwapa uwezo wa kujiamini;
Kipindi cha ujauzito mwanamke hua anapata hofu sana na kutojiamini na mwili wake, hua na wasiwasi kwamba mwili wake unaharibika hivyo kitendo cha mwanaume wake kuendelea kushiriki naye tendo la ndoa humpa kujiamini kwamba mwili wake bado uko kwenye hali nzuri na anapendwa.
Hupunguza msongo wa mawazo ; Kipindi cha ujauzito wanawake wengi huwaza sana kuhusu kesho yao…je swala la uchumi litakuaje? mwili wangu utakuaje? je ntapata jinsia nayotegemea? na kadhalika.. tendo la ndoa hutoa homoni ya upendo kwa jina la oxytocin, homoni hii hupunguza mawazo na kumpa amani mjamzito.
huongeza upendo na mshikamano kati ya wapenzi; Katika hali ya kawaida wanandoa wakikwazana wanaweza wakapatana kwa kushiriki tendo la ndoa tu, amani na upendo kipindi hiki ni muhimu sana kwani kuna mtoto anakuja ambaye anatakiwa kuzaliwa huku baba na mama wakiwa wanapatana.
Hukuandaa na uchungu ; Ukishiriki ndoa wakati wa tarehe zilizokadiriwa zimefika unapata homoni moja kutoka kwenye mbegu za mwanaume kwa jina la prostglandin, homoni hii huivisha mlango wa uzazi na kuanza kufunguka taratibu kujiandaa na uchungu.
hutibu tatizo la kukosa usingizi ; Wanawake wengi wajawazito hua na dalili mbalimbali za maumivu na kuumwa sehemu tofauti za mwili na msongo wa mawazo, hii huweza kuwakosesha usingizi kabisa..tendo la ndoa huweza kuwapa usingizi mzuri.
Hupunguza presha ya damu; Kipindi cha tendo la ndoa presha ya damu hushuka kwenye kiwango kizuri sana, hii ni muhimu sana kwa wanawake wenye hatari ya kupata kifafa cha mimba kama wanene sana, wenye kisukari au wenye historia za ugonjwa wa presha kwenye koo zao.
MWISHO;
Hakikisha unatumia staili za tendo la ndoa ambazo hazimuumizi mtoto na mama yaani hakikisha haulilalii tumbo hasa mimba ikiwa kubwa, kuna staili muhimu kipindi hiki kama kuangalia upande mmoja, mwanamke kuja juu, au mwanamke kuinama.
Jumatano, 7 Agosti 2019
AJABU YA MWANAMKE KISAIKOLOJIA Na.Hassan Issa
Wanawake ni binadamu wa ajabu sana katika uso huu wa Dunia yaani hawa watu ni next level, kuwaelewa ni ishu iliyowashinda hata wana falsafa, Newton na uwezo wake wote linapokuja suala la wanawake lazima atoke kapa na (ndio maana haieleweki hata kama akioa). Manabii na busara zao zote walishindwa kuwaelewa wakaishia kushauri ya kwamba tuishi nao kwa akili. Sasa najiuliza ni jambo gani unaweza fanya bila kutumia akili?, hapa ndipo napata ushahidi kwamba kumbe wanawake walishindikana tangu zama za mwanzo kabisa!. Wanasaikolojia wanasema kuwa kama utamuoa/kuishi na mwanamke mwenye miaka 25 basi itakuchukua miaka 25 mingine kumuelewa huyo mwanamke angaalau kwa 90% maana hawa kila siku hubadilika na kuwa wapya kimatendo na kifikra.
Mwanamke unaweza mnunulia BMW X6 akatoka nayo kwenda kutembea, akiwa njiani akaombwa lift na kijana akampa akipitia sheli hela ya mafuta ikawa haitoshi, yule kijana akaamua kumuongeza ata elfu 20 basi mwanamke huweza kubadili mawazo na kumuona yule kijana ni bora kisa tu kachangia mafuta kuliko wewe uliyenunua BMW X6, mfano akitoka hapo akapitia supermarket kununua bidhaa labda akapungukiwa kiasi mfano anadaiwa elfu 20, na yule kijana akasema hiyo ntalipa mimi basi basi hapo atasahau zile zawadi zote huwa unambebea na hiyo elfu 20 inaweza kumfanya awaze kumtunuku yule kijana penzi.
Mwanamke unaweza mpa hela akanunue nyama kilo 5 buchani, mwenye bucha akimuongeza robo tu hilo litamfurahisha kiasi kwamba anaweza kumpa mwenye bucha penzi na akusahau wewe ulieyota hela ya nyama kilo 5.
Mwanamke unaweza kumnunulia nguo, weaving, mafuta, perfume na urembo mzuri akavutia ila akipita mtaani akasifiwa na mwanaume kuwa kapendeza inaweza kuwa chanzo cha kumtunuku penzi na akakusahu wewe uliyegharamika na kufanya asifiwe!.
Mwanamke unaweza kumpa mimba na ukamhudumia mwanzo mwisho na familia ukalea kwa juhudi zako zote ila siku mkikosana anakwambia niache na watoto wangu, apo ashasahau kuwa wewe ndiye uliyempa mimba na kumlea yeye na watoto!
Mwanamke ndiye kiumbe pekee anayeweza kukupenda bila sababu ama kukuchukia bila sababu tofauti na viumbe wengine.
Mwanamke ndiye mwigizaji mkubwa ulimwenguni, anaweza kulia kwa furaha na akacheka kwa huzuni, bado hujawajua tu wanawake!
Mwanamke akisema ndio humaanisha hapana, na akisema hapana humaanisha ndio, pia anaweza kucheka bila kujua sababu lakini pia anaweza kulia pasipo sababu ya msingi ya kumfanya alie, hivyo chunga sana usijejichanganya!.
Mwanamke hupendi vutu vigumu na vyenye hatari mfano wanaume wenye nguvu, mlevi, muhuni (playboy), jambazi, mgomvi anayeogopwa hata na wanaume wenzie ila ukimuuliza anakuambia mie napenda kuwa na mwanaume mpole mwenye hofu ya Mungu tifauti na sisi wanaume tunavyopenda vitu vipole na vinyenyekevu na vyenye ukarimu, sasa wewe jifanye kumuamini mwanamke!
Jinsi unavyozidi kumpenda na kumthibutishia upendo wa dhati ndivyo unavyozidi kujiweka mbali nayeye, mwanamke hupenda migogoro isiyo na maana, ukijua hili ndoa haitokusumbua. Mwanamke hupendi utulivu kamwe!, usipomchokoa atakuchokoa tuu na usipomuendesha lazima akuendeshe yeye, Hawa viumbe hawana hiyana aisee!.
Mwanamke hupendi vitu vikubwa wala vidogo, kiufupi hana chaguo maalumu. Ukimnunulia gari sio garantii ya yeye kutulia nawewe bali anaweza kukusaliti hata na muosha gari wako. Ukimjengea nyumba nzuri na kumuwekea kila kitu sio njia ya kumteka kimahaba kwani anaweza kumtunuku penzi ata mtunza bustani wa nyumba yako.
Mwanamke hapendi ukweli, Ukimpa ukweli akija mwenye uongo basi we andika maumivu. Unaweza kuwa na elfu 50 ukamueleza ukweli kuwa "mke wangu leo hali mbaya chukua hii elfu 30,"... akatokea jamaa akamuongopea kuwa "Chukua hii elfu 15 ngoja nimesahau ATM card yangu nyumbani ikifuka saa 10 jioni ntakutumia laki 2 kwenye simu", Usishangae mkeo akakusaliti hata kabla ya hiyo saa 10 na iyo laki 2 asiione katu!.
Unamuoa hana ishu akiwa kwao amekaa tu, unaamua kumfungulia biashara hata ya duka unamjazia kila kitu. anatokea mshikaji mmoja kumuunga pale dukani kila siku na kumuachia soda tu na hicho kinakuwa kigezo tosha cha kuona mshikaji anamjali kwa kumuachia ya soda kila siku kuliko wewe uliyemfungulia duka zima na kinachofuata ni usaliti tu.
😂🙌🏽🙌🏽🙌🏽🙌🏽
Huu ni utafiti mdogo wa Mtanzania mmoja
Jumatatu, 5 Agosti 2019
ISHI LEO YAKO KITAALAMU
Habari za Leo ndugu zangu, napenda kuwapa makala hii Leo ilikujifungua kidogo pale tulipofungwa,
Wengi tumechanganywa na Mada Ya Leo na Tunajiuliza mmh innocent anataka kusena mini? Au nitaishi vipi kitaalamu? Basi majibu ya maswali yako utayaoata hivi punde,
Dunia ya leo nu Dunia iliyo jaa utandawazi, ni Dunia iliyo endelea pia tunasema ni Dunia iliyopiga hatua, Leo chochote ukitakacho unakipata tena kwa wepesi,
Swali; Nitaishije kitaalamu?.
Jibu lipo hivi;
1.Kuwa na ndoto inayo ishi katika maisha yako,
2.Anza kutengeneza njia za kufikia ndoto yako,
3.Jifunze zaidi namna ya kufikia malengo
4.Usikate tamaa juu ya ugumu unaoupitia.
5.Ishi kwa kufuata taratibu (mila na desturi) Za jamii inayo kuzunguka,(Jenga mahusiano mema)
6.Tatua matatizo ya jamii na yatumie kama fursa.(Tengeneza mtandao mzuri)
7.Tembea na kundi La watu wenye maono chanya,(Achana na mvuvu/mlalamikaji)
8.Zua mijadala ya kimaendeleo kukusanya fikra za wengine ili kutengeneza fursa,
9.Anza biashara yeyote kwa fedha yeyote uliyi nayo hata kama ni Kiduchu.
10.Fanya tofauti na wengine kwa ubora zaidi,
Hayo ni baadhi ta Mambo Muhimu ambayo tunasema ni ya kitaalamu katika safari ya mafanikio yako.
Hivyo nikutakie utekelezaji mzuri wa hayo machache na endelea kufuatilia makala zangu ujifuuze zaidi,
*ishi kitaalamu usiishi kizembe (Kivivu)*
Ni Mimi Mwalimu wako Innocent M Priscus,
NAMNA NZURI YA KUANDAA MPANGO WA BIASHARA
Biashara zote nzuri zinahitaji mpangilio. Panga vyema na utatengeneza pesa zaidi. Mpangilio wa biashara unakufanya uangazie malengo yako makuu. Unakutaarifu ulikotoka, umefikia wapi kwa sasa, na ni wapi unahitaji kuenda kama biashara.
Inaweza pia kukusaidia kupata mkopo kutoka benki, inasaidia watu kukukopesha pesa na inawaeleza watu unataka biashara yako iwe vipi katika muda wa miaka 3 mpaka 5.
Hatua ya
1: Muhtasari na maelezo ya biashara.
Moja ya vitu vya kwanza unachohitaji kufanya ni kuandika muhtasari wa biashara na maelezo. Hii itakusaidia wewe na wengine kuelewa nini unachotarajia kufanikisha:
Muhtasari wa Biashara : Nini unataka kufanya? Wapi? Vipi? Kwa kiasi gani?
Maelezo ya Biashara : Nini kinatokea leo? Nini kinaweza kutokea hapo mbeleni katika eneo lako? Unaweza kufanya nini? Unaweza kuifanya vipi? Kitatengeneza vipi pesa?
Hatua ya 2: Mpango wa uzalishaji
Hakikisha muda wote una kitu cha kuuza kwa mfano ng’ombe wa maziwa. Kama ng’ombe wako wote watazaa kwa wakati moja, hautakua na maziwa ya kuuza. Kama una ng’ombe mmoja anaetoa maziwa, nini kitatokea kama akiwa mgonjwa?
Mara nyingine ni vizuri kuwa na biashara zaidi ya moja. Jaribu kufuga kuku au kupanda mboga.
Hatua ya 3: Mpango wa Masoko
Angalia soko. Nini kinatokea katika soko kwaajili ya biashara yako leo? Hatua muhimu ni kutambua mnunuzi kwaajili ya zao lako, kuhakikisha unahudumia kuendana na mahitaji. Hii itahakikisha unapata rejesho katika uwekezaji wako.
Kuna Ushindani gani hapo? Kama una mshindani, unahitaji kufikiria jinsi unavyoweza kuwa tofauti na kutoa thamani nzuri kwa wateja wako. Utafanya nini kama mshindani akitokea?
Zingatia P 4 zifuatazo – Bei, Bidhaa, Ukuzaji na Mahali:
Uza kwa bei nzuri. Tambua kiasi majirani zako wanachouzia maziwa. Kama bei iko juu sana watu hawatanunua maziwa yako.
Bidhaa yako ni gani? Katika hili je maziwa ni safi na mabichi( Haijakaa).
Watu wanajuaje kama unauza maziwa? Unahitaji kutangaza . Bango/ Tangazo mlangoni? Kuwajulisha watu kanisani?
Wapi watu wanaweza kununua maziwa yako? Nyumbani kwako? Unapeleka? Kwenye OLX au mtandao wa kijamii?
Kwa taarifa zaidi kuhusu kujua masoko bonyeza hapa.
Hatua ya
4: Mpango wa kifedha.
Uzalishaji na utafutaji masoko unagharimu pesa. Unahitaji kiasi gani cha fedha? Je utahitaji mkopo? Una akiba ambazo unaweza kutumia?
Utahitaji kuandaa bajeti. Panga bajeti yako kukopa, kuweka akiba, kuwa na pesa za kuendesha na kukuza biashara yako, na kiasi gani unaweza kujilipa.
Hatua ya 5: Mpango wa kuendesha biashara
Jinsi gani biashara itaendeshwa siku baada ya siku? Je utahitaji watu wa kukusaidia? Je utahitaji kufanyia ukarabati vifaa vyako na je unahitaji usafiri?
Hatua ya 6: Mkadirio ya hatari
Matatizo inaweza kutokea wapi? Ni muhimu kuwaza kwa kina kuhusu hatari , kwa mfano; Utafanya nini kama mavuno ya mazao yako ni mabaya na kama ng’ombe wako akiwa mgonjwa
Jumatano, 2 Januari 2019
MWAKA 2019 NA MAFANIKIO YAKO
Naamini Kwa kipindi kirefu hatujaweka makala yeyote ila Sasa tunakuja NA mambo mazuuri kabisa MWAKA huu2019 "HERI YA MWAKA MPYA 2019" usisite kutufuatilia Hakika utafurah, Lilli shindikana 2018 litawezekana 2019