Jumanne, 15 Oktoba 2019

KAULI TANO ZA KUKUONGOZA UNAPOKUA KAZINI

Kila kazi ina muda na wakati wake kabla hujaanza kazi asubuhi jaribu kupitia haya kwa makini 

 A,Kuna maisha baada ya kazi unayoifanya, heshimu kipato chako na usimdharau mtu kwa nafasi uliyonayo,

 B,Fanya jambo kwa nafasi yako siyo kwa kuiga, angalia nafasi yako katika kusaidia na kufanya kitu Fulani,Kama mwenzako kafanya makubwa na huna uwezo was kufanya kama yeye usilazimishe,

 C.Penda kazi yako angalia ulipotoka na usifuate makundi, kumbuka kazi uliomba mwenyewe na ukafika mwenyewe marafiki uliowakuta kazini wasibadili tabia yako na kukufanya upotee kwani mwisho wa Sik kila mmoja atarudi alipotoka,

 D.Busara yako ikuongoze katika mambo yako kazini, kabla hujachangia chochote fikiria kwanza ubora na udhaifu was kile unachoenda kukiongea ndipo utoe hoja kukosoa au kuunga mkono,

 E. Tii mamlaka iliyoko juu yako, tii viongozi wako na Fanya kazi pasipo kuangalia udhaifu wao kwani hata maandiko matakatifu yanasema tiini mamlaka iliyo kuu kwani mamlaka zote zimewekwa na Mungu,

Kwa elimu na mafunzo mbalimbali ya namna ya kufanikiwa tucheki SMS/WhatsApp no: 0710843184
Mwl Innocent Massawe Priscus

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni