Habari,
Leo nakuletea Fursa za Biashara ambazo Tunaishi Nazo Tanzania,na wengi tumekua hatuzitumii.
Zipo Fursa nyingi katika sekta mbalimbali kama; Kilimo,uchuuzi,usindikaji,kutengeneza bidhaa n.k
Leo nakupa kwa uchache Fursa za biashara ndogondogo Tanzania ambazo unaweza kuzitumia na ukabadili maisha yako.
1.Kutengeneza Mifumo inayotumia mtandao, (APPS) Mifumo hii inaweza kuwa mahususi kwa Huduma mbalimbali kama starehe/burudani,Biashara,Huduma za kijamii n.k
2.Ufugaji; hapa tunaangalia Ufugaji mdogo wa Mbuzi wa kisasa,kuku chotara,samaki,sungura,unenepeshaji ng'ombe n.k
3.Kilimo Biashara; Kilimo hiki kinategemea na hitaji la watu ila best ni "Mboga za Majani" hiki ni Kilimo ambacho soko lake ni kubwa Tanzania, pia unaweza kulima Papai,Tangawizi,Miche ya miti,n.k Kikubwa endana na uhitaji wa eneo ulilopo,
4.Usindikaji; Pia unaweza kusindika Asali,Viungo mbalimbali,Mafuta yatokanayo na matunda,n.k Chukua malighafi mtaani na uiongezee thamani kisha irudishe sokoni,
5.Huduma za usafiri; Katika kipengele hiki nitazungumzia juu ya kukodisha usafiri kama pikipiki au baiskeli kwa maeneo ya vijijini, na mijini, Kuwa wakala wa kampuni/mtu kutafuta wateja (Dalali) n.k
6.Huduma za Miamala ya simu; Hii ni Fursa Muhimu pia kuwa Wakala wa Tigo,Vodacom,Airtel n.k kuweka na kutoa fedha kusajili line na kutatua changamoto za mtandao,
7.Huduma ya kibanda umiza; Namaanisha kibanda cha kuonyeshea Movies,Mipira mbalimbali ya TPL,Afcon,EPL,UEFA n.k Pia katika kibanda hiki unaweza kuwa na Huduma za kucharge simu,kuuza vocha na kuuza vinywaji baridi
8.Huduma ya Genge; Genge pia huweza kubadili maisha yako tengeneza Genge uza mbogamboga kama, Dagaa, samaki,mchicha,ndizi,matunda mengne kama maembe,machungwa pia boresha uza mikate, n.k
9.Huduma ya Bites (mjini); Bites ni muhimu hasa maeneo ya stand za mabus unaweza tengeneza sehem ya kuuza vikorokoro mbalimbali vya kukaanga na uka make money, Hapa yaweza kuwa,Karanga,popcon,kuku,vusheti,crips,chips,n.k
10.Huduma ya maji,juice na urembo vituo vya mabus; Wapo wengi wanauza hivi vitu na ukitulia na kufanya Biashara vizuri hakika hutabeba lile boksi LA maji miaka miwili lazima uwe na mtaji
All the best
Kwa msaada Kibiashara nitafute hapa,
0710843184
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni