Leo nakuletea aina tatu za watu katika tofauti katika kipato pamoja na tabia zao,
,Katika maisha yetu ya kila Siku tuna aina tatu za watu kulingana na kipato chao ambao ni hawa wafuatao;
A,Watu wenye kipato cha juu,
B,Watu wenye kipato cha kati,
C,Watu wenye kipato cha chini,
Hayo ndiyo makundi makuu ya kipato katika Dunia hii ya Teknolojia, Kiufupi tutazame sifa/tabia za kila kundi,
A.WATU WENYE KIPATO CHA JUU;
za hawa hutumia kipato walichonacho kuzalisha kipato kingine, Mfano anamoliki Kampuni kubwa fedha anazozipata huzitumia kufungua kampuni nyingine ndogo.
Pia hawa huweka akiba na kwa kawaida huendelea kukua na kufanikiwa zaidi kutokana na kuwa na vyanzo vingi vya mapato,
Tabia nyingine huwa ni wavumilivu, wenye subira, wanajali na wapo makini katika kusimamia miradi yao vilevile wana uhusiano mzuri sana na jamii inayo wazunguka,
Tabia ya mwisho watu hawa hutumia muda wote 24 hrs kuzalisha na huwa na dharura nyingi wanapo alikwa katika sherehe au matamasha kutokana na huwa bize sana,
B.WATU WENYE KIPATO CHA KATI
Hawa tunao kwa wastani katika mazingira yetu na huwa wana tabia zinazo shabihiana na za wale wenye kipato cha juu na maranyingi huweza kufikia kipato cha juu kirahisi, Hawa hupenda kuzalisha Mali pia baadhi hupenda starehe za wastani na muda mwingi huutumia katika kuzalisha na starehe, ni rahisi sana hawa kutajirika pia ni rahisi kufilisika,
Katika hatua hii wengi huwekeza katika asset mbalimbali kama mashamba/viwanja nyumba/majengo n.k
C.WATU WENYE KIPATO CHA CHINI
Hawa ndio wenye kundi kubwa Duniani, watu hawa wana sifa nyingi zinazowafanya kuendelea kuwa maskini;
1.Wavivu kufanya kazi na hupenda kuajiriwa kuliko kujiajiri wenyewe hulala sana na hupenda starehe, hunununa mapambo mengi ya ndani na vikorokoro vingi vya nyumbani,pia hawana akiba na hufanya matumizi makubwa bila mipango, humiliki vitu vya anasa visivyozalisha kama nguo,n.k
2.Kwakawaida watu hawa hawatumii kipato chao kuzalisha kipato kingine hivyo hubaki katika umasikini wao daima,
MWISHO; Kila mtu alizaliwa maskini lakini siyo kila MTU atakufa maskini, hii ni kutokana na mfumo wa maisha yako, Badili mtazamo wako sasa na Ishi kitaalamu ukiiona kesho iliyo bora kuliko Leo,
Kwa msaada wa kijasiriamali wasiliana nasi
0710843184/0753352264
Mwl wako INNOCENT M PRISCUS
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni