Usikae bila shughuli yeyote
Epuka uvivu, Buni Kitu kitakachokupa fedha yaani shughuli ambayo ita kukeep busy, kwa kiwango kidogo
Usidharau ulivyo navyo
Haijalishi ni kidogo kiasi gani focus katika maono chanya kipende,kiheshimu, ongeza ubunifu na ukikuze,
Acha visingizio
Mafanikio ya mtu humtegemea yeye kwa 90%, Mafanikio yako yapo ndani yako, Usimlaumu au kumsingizia mtu.
Usiahidi uongo na usidhulumu MTU
Ukitoa ahadi hakikisha unatekeleza na pia tenda haki, hapa tunazungumzia "Mahusiano" Jenga mahusiano mazuri na jamii inayokuzunguka kwani jamii yako ndiyo maendeleo yako
Usiwe tegemezi wa mawazo
Usiishi kwa mazoea,kufuata mkumbo au kufuata wanachotaka wengine, "Fanya unacho amini kuwa ni sawa"
Usikate tamaa
Unapokutana na magumu pambana nayo, unapo anguka simama, unapokosea jifunze, songa mbele na kamwe usiwe na woga,
Nikutakie utekelezaji mwema,
Mwl Massawe,
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni