Jumatatu, 5 Agosti 2019

ISHI LEO YAKO KITAALAMU

Habari za Leo ndugu zangu, napenda kuwapa makala hii Leo ilikujifungua kidogo  pale tulipofungwa,
     Wengi tumechanganywa na Mada  Ya Leo na Tunajiuliza mmh  innocent anataka kusena mini? Au nitaishi vipi kitaalamu? Basi majibu ya maswali yako utayaoata hivi punde,
       Dunia ya leo nu Dunia iliyo jaa utandawazi, ni Dunia iliyo endelea pia tunasema ni Dunia iliyopiga hatua, Leo chochote ukitakacho unakipata tena kwa wepesi,
Swali; Nitaishije kitaalamu?.
Jibu lipo hivi;
1.Kuwa na ndoto inayo ishi katika maisha yako,
2.Anza kutengeneza njia za kufikia ndoto yako,
3.Jifunze zaidi namna ya kufikia malengo
4.Usikate tamaa juu ya ugumu unaoupitia.
5.Ishi kwa kufuata taratibu (mila na desturi) Za jamii inayo kuzunguka,(Jenga mahusiano mema)
6.Tatua matatizo ya jamii na yatumie kama fursa.(Tengeneza mtandao mzuri)
7.Tembea na kundi La watu wenye maono chanya,(Achana na mvuvu/mlalamikaji)
8.Zua mijadala ya kimaendeleo kukusanya fikra za wengine ili kutengeneza fursa,
9.Anza biashara yeyote kwa fedha yeyote uliyi nayo hata kama ni Kiduchu.
10.Fanya  tofauti na wengine kwa ubora zaidi,

Hayo ni baadhi ta Mambo Muhimu ambayo tunasema ni ya kitaalamu katika safari ya mafanikio yako.
  Hivyo nikutakie utekelezaji mzuri wa hayo machache na endelea kufuatilia makala zangu ujifuuze zaidi,
*ishi kitaalamu usiishi kizembe (Kivivu)*
Ni Mimi Mwalimu wako Innocent M Priscus,

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni