Jumatatu, 31 Oktoba 2016

MAGONJWA YA KUKU NA TIBA ZAKE.

🐓🐓🐓🐓
UTANGULIZI
   Kuku kama wanyama wengine hushambuliwa na magonjwa mbalimbali ambayo mengine yanatibika kwa dawa na mengine hayana tiba bali kuku hupewa chanjo maalumu ambayo huzuia magonjwa hayo.Leo nitawaeleza baadhi ya magonjwa ambayo hushambulia kuku mara kwa mara na ambayo ni chanzo cha kuwakatisha tamaa wafugaji wa kuku.

A.) MAGONJWA YANAYOHITAJI CHANJO
     1> GUMBORO
                Ugonjwa huu husababishwa na virusi.
     
      DALILI ZA UGONJWA
    -Kuku kuzubaa na kulundikana, pamoja na kusinzia
    -Kuku kuharisha
    -Kuwa na vifo vingi kwa kuku

     TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba,,Kuku wakipewa Dawa za oxytetracycline hupunguza vifo.

    KINGA
wakinge kuku wapo kwa kuwapa chanjo ya gumboro (Gumboro vaccine)

   2> MAHEPE (Marecks)
             Ugonjwa huu husababishwa na virusi

        DALILI
     -Kuku hupata ulemavu na vifo vya mara kwa mara.
  
    TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba

    KINGA
Chanjo hutolewa kwa vifaranga wenye umri wa siku moja,vifaranga hupewa chanjo ya mahepe (Marecks vaccine)

   3>NDUI YA KUKU (Fowl Pox)
            Ugonjwa huu husababishwa na virusi.

     DALILI
    -Kuku hupatwa na vidonda kichwani.
    -Kuku hupata uvimbe mweupe kwenye mdomo na kushindwa kula.

      TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba.

   KINGA
Chanja kuku wako wa siku 60-90 kwa chanjo ya Ndui ya kuku (Fowl pox vaccine).

  4>MDONDO (New castle)
           Ugonjwa huu husababishwa na virusi
 
   DALILI
  -Ugonjwa huu hutokea kwa ghafla na kuenea kwa haraka
  -Vifo vya kuku huwa vingi
  -kuku hupumua kwa  shida
  -Kuku hupooza na kulemaa miguu
  -Kuku hupinda shingo yake
  -Kuku hupunguza kutaga mayai
  -kuku huarisha
  -Kuku Kuzunguka zunguka na kutembea kinyume nyume.

   TIBA
Hauna tiba

    KINGA
  Chanja vifaranga wako na kuku wako kwa chanjo ya Mdondo (New castle vaccine) na urudie chanjo hii kila baada ya miezi mitatu.

B.)MAGONJWA YANAYOTIBIKA KWA DAWA

    1>KUHARA DAMU (coccidiosis)(Koksidiosisi
             Ugonjwa huu husababishwa na virusi.

    DALILI
-Kuku huzubaa na kujikunyata
-Kuku kuharisha kinyesi chenye damu au kinyesi cha kahawia
-Kuku hudhoofika,manyoya huvurugika na kulegea mabawa na kuonekana kama wawevaa koti
-Kuku hupungukiwa homa ya kula
-Vifo huwa vingi kwa vifaranga

TIBA
Wape kuku wako dawa kama Esb 3, Amprolium, au Basulfa.

KINGA
Zingatia usafi wa banda la kuku na usiruhusu unyevuunyevu katika banda la kuku,

   2>HOMA YA MATUMBO(Fowl typhoid)
        Husababishwa na bakteria

   DALILI
   -Kuku hupata homa kali
   -Kuku huarisha kinyesi cha kijani au njano
   -Vifo huwa vingi hasa kwa vifaranga wenye wiki 1-2
   -Kuku huzubaa,kuvimba viungo vya miguu,kuchechemea,kukosa hamu ya kula
   -Kuku wanaotaga hupunguza utagaji,hutaga mayai yenye ganda laini na hupata vifo vya ghafla

  TIBA
  Dawa za oxytetracycline kama Furamax,Typhoprim hutibu ugonjwa huu.

KINGA
  Hakikisha usafi wa banda na vyombo vya chakula na maji kwa kuku.
  Tenganisha kuku wagonjwa na wazima

C)MINYOO
Hushambulia kuku wote wakubwa na vifaranga

DALILI
-Kuku hukonda
-Kuku huarisha
-Kuku hukohoa
-Kuku hupunguza utagaji
-Kuku hudumaa katika ukuaji/hawakui vizuri
-Kuku hupungua uzito

TIBA
Tumia dawa za minyoo kama piperazine

KINGA
Wapewe dawa za minyoo mara kwa mara kila baada ya miezi mitatu

D)VIROBOTO/CHAWA/UTITIRI
   Hushambulia sana vifaranga na hutokea vifo kwa wingi kwa vifaranga Kwa kuku wakubwa tatizo halionekani kwa sana lakini nao huathiriwa sana.

DALILI
-Kuku kutochangamka
-Ukuaji mdogo wa kuku
-Kuku kutotaga na kuhatamia vizuri kutokana na kusumbuliwa na chawa,utitiri au  viroboto
-Viroboto huonekana kuganda machoni wakinyonya damu

TIBA
Tumia dawa za unga kama sevin dust 5% ,Malathion ,akheri powder kwa kuku wote na mabanda yao.

KINGA
Boresha usafi wa mabanda ya kuku.

E)UKOSEFU WA VITAMINI A
    huathiri sana kuku wadogo.

DALILI
   -Kuku huvimba macho na kutoa uchafu mzito kama  sabuni ya kipande iliyolowana.
   -Mara nyingi  ugonjwa hujitokeza baada ya kipindi kirefu cha kiangazi

TIBA
wape kuku wote dawa za vitamini.

Jumatano, 26 Oktoba 2016

HIZI NDIZO SIFA ZA MWANAMKE WA KUOA

   Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha.
     Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachowezakuwafanya wakapata wachumba niuzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.
     Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa.
Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.

1. MWEYE MAPENZI YA KWELI
Lengo kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto mara ndio wamekuwa furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake.
Mwanamke asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingiutamuona macho yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.
Kwanini wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.
Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.
Si hivyo tu pia asilimia kubwa ya maisha ya ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha ya raha mustarehe.

2. WENYE TABIA NZURI
Tabia njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja sualana kuoa tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani utaambiwa anatabia mbaya.
Naweza kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.
Si hivyo tu wapo wanaume ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.

3. WENYE UCHU NA MAENDELEO
Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani ‘golikipa’. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini.
Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.

    4. WASIOPENDA MAKUU
Kuna wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila wikiendi utamsikia “leo tunakwenda wapi dear?”
Akimuona rafiki yake kanunua simuya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama ya Grace’. Ukienda naye Pub anakuambia,”mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’. Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho nacho na usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.
Wanawake kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa kuwaoa. Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?’ hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu fulani.’
Wanaume ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.
Kuna wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leoamemletea hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema.
Sisemi kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitajiupo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulaniwakati inawezekana uwezekano haupo.

         5. WAVUMILIVU
Wapo wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.
Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotokea kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?
Uvumilivu kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.
Licha ya kupenda kuoa wanawake amabo wana tabia hizo nilizozitaja hapo juu, wanachukizwa sana na wanawake ambao wanavijitabia vidogo vidogo ambavyo kimsingi havikubaliki katka jamii.
Tabia hizo ni kama wambea, wasio wakweli na wawazi, wasioridhika, wagumu kusamehe na wapesi wa kuchukia, wagomvi na wenye roho ya kwanini.
Utafiti huu umefanyikwa kwa baadhi ya wanaume ambao wanatarajia kuoa wanawake ambao wanaoishi katika maeneo mbalimbali
Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.